Wednesday, September 9, 2015

HOFU YATANDA, SILAHA ZA KIVITA KUKAMATWA

Silaha zilizokamatwa zikioneshwa kwa wandishi wa habari.
Na Timu ya Uwazi, Mkuranga-GPL
HOFU kubwa imetanda kwenye Kijiji cha Mamndi Mkongo kilichopo Wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani kufuatia Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa  kushirikiana na wale wa mkoa huo kunasa silaha  nyingine za kivita zikiwa zimefukiwa kwenye shimo msituni.
Tukio hilo  la unasaji wa silaha lilifanikiwa Agosti 29,  mwaka huu  katika msitu  mmoja uliopo  katika kijiji hicho  kilichopo umbali wa kilomita 23  kutoka mjini Mkuranga.
NI KAWAIDA YA UWAZI
Baada ya Uwazi kuzipata taarifa za polisi kuzinasa silaha hizo lilifunga safari hadi kwenye eneo la tukio na kushuhudia shimo ambalo silaha hizo za kivita zilifukiwa kwa utunzaji wa siri.
Silaha za kigaidi zilizokamatwa.
MKUU WA MGAMBO ASIMULIA
Katika Mahojiano maalum na kiongozi wa wanamgambo wa  Kata  ya Bup iliyopo kwenye kijiji hicho, Mussa Mohammed Koti alisema wamekuwa  wakifanya doria  katika mazingira magumu na hasa baada  ya vikosi  vilivyokuwepo kuondoka. Awali huku kulikuwa na vikosi maalum vya ulinzi na usalama.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova akizungumza na wandishi wa habari.(P.T)

No comments:

Post a Comment