Thursday, October 29, 2015

Shukrani zangu za dhati kwa wote

Kwanza napenda kusema Hongera sana Mtanzania.

Kwa Niaba Ya Rais wetu Mpya Naomba kuwashukuru vijana wote waliopambana kwa niaba ya CCM na Mgombea wetu Mpaka kufikia hatua hii.

Pia naomba kutoa shukrani za dhati kwa wale wote mliokuwa mkiwaelimisha vijana juu ya kujiepusha na fujo, matusi, na kejeli mitandaoni, naamini sasa wamejifunza.
Sisi sote ni waTanzania, Rais wetu ni Mmoja, na tunakiri kuwa Upinzani umekua japo demokrasia imeamua.
‪#‎TanzaniaKwanza‬
#HapaKaziTu



Mungu Ibariki Tanzania

No comments:

Post a Comment