Thursday, December 3, 2015

PICHA: Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipofanya ziara ya kushtukiza leo bandari ya Dar es salaam na Shirika la reli..

PICHA: Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipofanya ziara ya kushtukiza leo bandari ya Dar es salaam na Shirika la reli... Akizungumza na Mkurugenzi Mkuu TRL, Mhandisi Elias Mshana, Waziri Mkuu alisema amefika kwenye shirika hilo ili kujifunza utendaji wao kazi lakini anazo taarifa za wao kupewa fedha na Serikali kiasi cha sh. bilioni 13.5/- ili waendeleze miundombinu ya reli lakini hawakufanya hivyo. “Nia ya kuwapa fedha hizo ilikuwa ni kuboresha miradi ili muweze kujiendesha kibiashara lakini nyie mkaamua kujilipa wenyewe,” alisema.
“Ninazo taarifa kuwa baada ya hapo, mlikopa sh. bilioni 3 kutoka benki ya TIB ili kuendesha miradi ya shirika lakini badala ya kufanya miradi, fedha hizo mkaamua nazo kujilipa mishahara. Sasa sijui mnarudishaje huo mkopo wakati hakuna mradi wowote uliofanyika,” alihoji bila Waziri Mkuu kupata majibu.













No comments:

Post a Comment